Baada ya Kocha NABI Kuchoshwa na Pasua Kichwa Morrison Aamua Kumpiga Chini Safari ya Tunisia

 

Baada ya Kocha NABI Kuchoshwa na Pasua Kichwa Morrison Aamua Kumpiga Chini Safari ya Tunisia

Kocha Mkuu wa Yanga, Nasreddine Nabi amesema uwezekano wa winga wake Bernard Morrison kusafiri na wenzake kwenda Tunisia kuwafuata wapinzani wao US Monastir ni mdogo sana kutokana na kile alichokisema ameumia.

Nabi alisema Morrison aliumia akiwa kwao Ghana na kwamba atakuwa nje kwa muda mrefu, lakini akawashusha presha mashabiki wa timu hiyo kuwa Yanga itaendelea na maisha kama kawaida.

“Sioni uwezekano wa Morrison kusafiri na timu, nafikiri huyo ndio mchezaji tunayeweza kumkosa katika safari hii lakini nimekueleza kuwa nafasi yake itazibwa,” alisema Nabi na kuongeza;

“Kuna mpango tumeshaanza kuufanyia kazi jinsi ya kutafuta mtu muafaka wa kuziba nafasi yake na anaweza kuwasapraizi watu siku ya mchezo wetu wa kule.”

Baada ya Kocha NABI Kuchoshwa na Pasua Kichwa Morrison Aamua Kumpiga Chini Safari ya Tunisia

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad