Harmonize Anateswa na Upwiru "Sijafanya Mapenzi kwa Miezi Mitatu"



Msanii wa Bongofleva toka Konde Music, Harmonize amedai kwamba mara yake ya mwisho kufurahia tendo la ndoa ni wakati alipokuwa kwenye mahusiano na Kajala Masanja.


Akizungumza kupitia ukurasa wake wa Instagram siku ya Ijumaa, Konde Boy aliweka wazi kuwa hajashiriki mapenzi kwa miezi mitatu sasa.


Hata hivyo, hajaonyesha majuto yoyote ya kuwa bila mpenzi sasa kwani anadai hilo limemfanya kuwa na nguvu zaidi.


“Maisha ya kuwa single yanakufanya kuwa na nguvu, miezi mitatu sijawahi kushiriki mapenzi. Najua hamuwezi kuamini hili,” alisema Harmonize.


Ikumbukwe ni takribani miezi mitatu tangu Harmonize kuachana na Kajala Masanja ambaye waliwahi kuachana na kurudiana.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad