Vijana 147 waliojiunga na JKT wakutwa na VVU

 

Vijana 147 waliojiunga na JKT wakutwa na VVU

Vijana 147 kati ya 67,299 waliojiunga na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kwa mujibu wa sheria katika kipindi cha miaka mitatu wamekutwa na maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU).


Takwimu hizo ni sawa na asilimia 0.22 kwa vijana waliomaliza kidato cha sita nchini na ambao waliitwa kujiunga na JKT katika kipindi cha miaka hiyo 2019, 2020 na 2021.


Hayo yamo katika taarifa ya Kamati ya Bunge ya Masuala ya Ukimwi kwa kipindi cha Februari 2022 hadi Februari 2023 iliyowasilishwa bungeni jijini Dodoma jana Ijumaa, Februari 3, 2023.


Taarifa hiyo, iliwasilishwa na Mbunge wa Manyoni Magharibi, Yahaya Massare akieleza hali bado si nzuri katika maambukizi mapya ya VVU ingawa kitakwimu kumekuwa na upungufu kwa kila mwaka.


Kamati hiyo imependekeza mkakati wa kupima na kuzuia maambukizi mapya ya VVU uongezwe. Pia pawepo na juhudi za makusudi katika lishe kwa wafungwa wenye maambukizi hasa Gereza la Isanga jijini Dodoma.


Kwenye taarifa hiyo, inaonyesha mwaka 2019, vijana waliojiunga JKT walikuwa 20,413 huku 60 wakikutwa na maambukizi wakati 2020 walijiunga vijana 21,383 na maambukizi yalikuwa kwa vijana 45 na mwaka 2021 walijiunga vijana 25,503 na 42 kati yao ndiyo walikutwa na VVU.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad