Bomu lililotegwa kwenye keki laua bwana harusi na kaka yake

 


Mwanaume mmoja aliyefunga ndoa hivi karibuni amefariki pamoja na kakake baada ya mfumo wa ukumbi wa michezo nyumbani waliopokea kama zawadi ya harusi kulipuka.


Polisi wanasema zawadi hiyo iliwekwa bomu ambalo lililipuka muda tu ilipowekwa katika umeme.


Wakati bwana alifariki hapo hapo, kaka yake alifariki kutokana na majeraha wakati wa matibabu.


Polisi walisema kuwa bomu hilo lilidaiwa kutumwa na aliyekuwa mpenzi wa bibi harusi ambaye alikuwa na hasira dhidi yake kwa kuolewa na mume mwingine.


Mshtakiwa, ambaye ametambuliwa kama Sarju Markam kutoka jimbo jirani la Madhya Pradesh, alikamatwa Jumanne. Kwa kuwa bado yuko kizuizini, hajatoa kauli yoyote.


Wengine wanne, akiwemo mvulana miezi 18, walijeruhiwa katika mlipuko huo, ambao ulifanyika tarehe 3 Aprili nyumbani kwa bwana harusi katika wilaya ya Kabirdham katika jimbo la kati la India la Chhattisgarh.


Polisi walisema Bw Markam, 33, alikuwa na uhusiano na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 29 na alikuwa akisisitiza kuwa awe mke wake wa pili.


Lakini familia ya mwanamke huyo ilikataa kupanga ndoa yake mahali pengine.


Polisi walisema mlipuko huo ulikuwa mkubwa kiasi kwamba kuta na paa la chumba hicho zilianguka kutokana na athari zake.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad