Leo Aprili 4, 2023 Wabunge kwa kauli moja wamempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuimarisha demokrasia nchini na kukuza diplomasia ya uchumi.
Awali Wabunge walipata nafasi ya kuchangia azimio hilo na kulipitisha ambalo lililowasilishwa na Mbunge wa Biharamulo Magharibi, Mhandisi Ezra Chiwelesa mara baada ya kipindi cha Maswali na Majibu wakati wa Kikao cha Kwanza cha Mkutano wa Kumi na Moja kilichoanza leo Mjini Dodoma.