Beki Kisiki wa Simba Kuondoka Simba, Kisa Kizima Hichi Hapa


UJIO wa beki wa kati kutoka Burkina Faso, Mohamed Ouattara ndani ya Simba umemfanya Mkenya Joash Onyango kupigwa benchi na Kocha Zoran Maki kiasi cha kukosa mechi mbili za awali za Ligi Kuu Bara sambamba na ile ya Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga.

Kumbe kitendo hicho cha kukalishwa benchi, kinamuuma Mkenya huyo na sasa amepanga kutuma maombi ya kutaka kuvunjwa mkataba ili asepe zake sehemu ambayo itamfanya acheze kama ilivyokuwa kabla ya ujio wa Kocha Maki na Ouattara.
Ouattara ambaye amesajiliwa kwa mapendekezo ya Zoran aliyefanya naye kazi katika klabu kadhaa ikiwamo Al Hilal ya Sudan na Wydad Casablanca ya Morocco ameingia kikosi cha kwanza akitengeneza pacha na Henock Inonga na kumng’oa Onyangoi.
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad