Feisal Salum 'Natokwa Machozi ya Furaha'


Mchezaji wa klabu ya Yanga na Timu ya Taifa ya Tanzania, Feisal Salum, ameeleza kuwa haamini anachokiona na anatokwa na machozi ya furaha kwa mapenzi makubwa ya Watanzania juu yake.

“Siamini ninachokiona, natokwa na machozi ya furaha kwa mapenzi makubwa ya Watanzania juu yangu. Mimi ni kijana mwenye nidhamu na busara ni vile nimeamua kunyamaza na kwenda CAS.
.
“Ninachokifanya ni kutetea Haki yangu ambayo nimeikosa hapa, lakini sio kwangu tu bali kwa wachezaji wote wazawa ambao hawasemi na wanasaini mikataba bila kujua. Endeleeni kunichangia nikapate haki na kutengeneza misingi kwa wazawa wengine na thamani zao.
.
“Wale mnaonipigia Simu siwezi pokea simu zote sababu simu ni nyingi sijawahi kuona, endeleeni kunichangia ndugu zangu”.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad