Daraja la Kigamboni Kuanza Kutumika Bure, Mbunge Afunguka Kwa Uchungu

Kuhus Daraja la Kigamboni Kuanza Kutumika Bure
Daraja la Kigamboni



Mbunge wa Kigamboni, Dkt. Faustine Ndugulile ameiomba Serikali kuondoa tozo za daraja la Nyerere ili Wananchi wa Kigamboni wapate ahueni ya maisha kwa kuwa gharama za maisha zimekuwa kubwa zikichangiwa na bidhaa zinazoingia Kigamboni.

Dkt. Ngugulile ameyasema hayo leo May 23, 2023 Jijini Dodoma akichangia mjadala wa Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024.

“Hoja ya Wananchi wa Kigamboni bado iko palepale, Wananchi wa Kigamboni ni walipa kodi wa nchi hii, michango yao na kodi zao zinachangia katika ujenzi wa madaraja mengine nchini lakini Wananchi Kigamboni ndio pekee katika nchi yetu ambao wao pekee wanachangia katika kuingia na kutoka Kigamboni hivyo wamenituma kusisitiza hoja yao ya kutaka tozo zile ziondolewe ili wapate ahueni ya maisha”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad