Wafanyabiashara wa Kariakoo Wagoma Kumfuata Waziri Mkuu Dodoma




Ni baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, #AmosMakalla kuwataka kupeleka malalamiko yao kwa Kassim Majaliwa ambaye anatarajiwa kukutana na Uongozi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mawaziri husika na Kamati ya Wafanyabiashara ili kutafuta suluhu ya mgomo huo

Makalla amefika katika Soko Kuu la Kariakoo baada ya Wafanyabiashara kugoma kufungua Biashara huku wakitoa malalamiko kadhaa ikiwemo madai ya uwepo wa utitiri wa kodi.

Wakizungumza baada ya Mkuu wa Mkoa kuondoka eneo la Kariakoo, Wafanyabiashara wamesema wanahitaji kuonana na Rais #SamiaSuluhu kwa ajili ya kutoa kero zao huku wakisisitiza kuendelea kufunga Maduka yao

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad