Waganga wa Jadi 10 Wapelekwa Kigoma Kupambana na Wachawi




Wananchi wa Kijiji cha Sunuka, Wilaya ya #Uvinza wameshirikiana na Serikali ya Kijiji kuchukua Waganga wa Jadi zaidi ya 10 kutoka #Sumbawanga ili kukagua Wachawi ndani ya Kijiji chao wakidai ni chanzo cha utitiri wa 'Vifo Tatanishi' vya vijana

Baadhi wa Wananchi walikusanyika na kuandamana barabarani wakiimba “Tumechoshwa na uchawi” huku wakiunga mkono mpango huo wa Viongozi wao wa Kijiji

Akizungumzia hali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Uvinza, Dinah Mathamani aliyezuiliwa kuingia Kijijini hapo kwa kuwa anapinga mpango wa kuleta Waganga hao, amesema “Suala tulishalizuia tangu wiki iliyopita, hao wanaojiita Waganga wanatakiwa kuondoka katika wilaya yetu. Hatua kali zitachukuliwa dhidi yao na Viongozi wanaoshirikiana nao.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad