Zari Hassan na Mume Wake Kubeba Mimba Kupitia Kwa Mwanamke Mwingine

zari hassan and Shakib
zari hassan and Shakib



Zari ambaye ni mama wa watoto 5, amesema Shakib ana mtoto mmoja tayari, Ila Zari amesema kwasasa wao ni wanandoa hivyo wanataka kuongeza watoto kwani yeye binafsi Zari anataka kuwa mama wa watoto 10

Zari amesisisitiza kuwa yeye kuongeza watoto wengine watano anaweza kubeba mimba mwenyewe, kubebewa mimba na mtu mwingine(surrogate) na pia kama kuna njia nyingine zaidi ya hizo ya kupata mtoto hatasita kuitumia ilimradi tu afikishe watoto 10 anaowataka na haoni tatizo kwani yeye binafsi ametokea kwenye familia kubwa.

Zari ameyasema hayo katika mahojiano na vyombo vya habari nchini Uganda na si mara yake ya kwanza kusema anataka watoto kumi

Lakini kwa umri wake 42 hajaweka wazi kama alishachukua hatua mapema mayai yake ya uzazi kuvunwa na kuhifadhiwa(egg freezing) ili isiwe shida yeye kuongeza watoto wengine 5 muda wowote anaotaka siku zijazo sababu ya umri wake unakoelekea(biological clock ticking)

Na baada ya hapo, kilichofuatia katika show ya Netflix Zari alimjia juu Diamond kwa madai ya kumueleza Fantana kuwa Zari anataka waongeze watoto. Hata hivyo, Zari alipomuweka Diamond mtu kati, Diamond alikana kumueleza Fantana huku Zari akimuuliza Mond kama akiamua kuzaa nae tena je kuna wa kumzuia ambapo Mond alijibu hakuna, kisha Zari kuibukia tena mtadanoni kumtungua Mond mwanzo mwisho

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad