DJBrownskin Aliyeshuhudia Mkewe Akinywa Sumu na Kufa Akamatwa na Polisi


Jeshi la Polisi Nchini #Kenya, linamshikilia kwa mahojiano, #DJBrownskin (Michael Macharia Njiiri) anayedaiwa kurekodi tukio ambalo limetajwa kuwa ni kosa la kusaidia kuua, kinyume na Kifungu cha 225 (c) cha Kanuni ya Adhabu

Upande wa Upelelezi umesema DJ huyo alimuacha Mkewe bila kuchukua hatua zozote kuzuia kitendo hicho, hali iliyosababisha kifo cha #SharonNjeri. Aidha, imedaiwa aliitwa Polisi mara 3 tangu Januari 2023 lakini hakuwahi kuitikia wito hadi alipokamatwa

Brownskin yuko mahabusu katika kituo cha #Kasarani, akichunguzwa kwa kushuhudia mkewe Sharon Njeri (24) akijiua kwa kunywa Sumu mbele yake na Watoto wao, usiku wa kati ya Julai 29 na 30 Mwaka 2022.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad