Hersi Afunguka Tena "Sintobadilika Suala la Fei Toto, Msimamo wangu ni Ule Ule"


Rais wa Klabu ya Yanga, Mhandisi Hersi Ally Said amesema "Vikao halali vilivyojadili suala la #FeiToto ni vile vya Kamati ya TFF ambavyo vimetoa maamuzi kuwa Fei anatakiwa kuendelea kubaki Yanga, mimi na Makamu wangu tulizungumza naye binafsi lakini haikuwa mazungumzo rasmi"

Akizungumza na Wasafi FM, Hersi amesema "Sijawahi kuwa na shida na #Feisal na nimewahi kumwambia yeye mwenyewe hivyo, nimeshangaa kuona alichokizungumza kuhusu Mimi. Pia, hili suala si jambo la kihisia, linahusiana na misingi ya Kazi na misingi ya Taasisi"

Ameongeza "Watu wanasema ni Kijana mdogo anatafuta Maisha tumuachie, hili sio suala la hisia. Mimi kama Rais wa Klabu nasimamia Misingi ya #Yanga na kuheshimu makubaliano ya Taasisi, nitasimama pale na siwezi kubadilika"

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad