Mbowe Afunguka Kwa Uchungu Sakata la Bandari Kubinafsishwa Kwa DP World




Akizungumza kutoka Berlin Ujerumani, Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Freeman Mbowe amesema Masharti ya Mkataba huo yanaonesha kuwa endapo kutakuwa na ulazima wa kuvunja Mkataba itabidi uamuzi utolewe na Mahakama ya Usuluhishi ya Kimataifa

Amesema DP World wanataka kupata haki ya kuendeleza, kuendesha na kuboresha Bandari zote za Baharini na Maziwa yote, kitu ambacho ni hatari kumwachia mtu mmoja kuhodhi maeneo hayo muhimu. Hali hiyo inaonesha Serikali haijapata funzo ilipobinafsisha Shirika la Reli, TANESCO, ATCL na Mashirika mengine

Aidha, ameongeza kuwa Mkataba umeanza kutekelezwa kwa shughuli za awali baada ya kusainiwa wakati Bunge halijaupitia na kuridhia, hivyo Bunge linatumika kwasasa kwenda kupitisha tu na halina mamlaka ya kubadili chochote

Vipi Mdau, una maoni gani kuhusu suala hili?

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad