Mwanamume Aliyebadilisha Jinsia na Kuwa Mwanamke Apachikwa Mimba

 

Mwanamume Aliyebadilisha Jinsia na Kuwa Mwanamke Apachikwa Mimba

Mwanamume aliyebadili jinsia kutoka West Virginia amekaidi uwezekano huo na kukubali kuwa mama.


Ash Patrick Schade, 30, ambaye aliamini kuwa ni tasa, alijipata mjamzito baada ya kujamiana na mwanamume waliyekutana kwenye Grindr mnamo Januari 2020.


Baada ya hisia zake kubadilika na kutokuwa kama kawaida, Schade alipima ujauzito mnamo 2020, na mshtuko wake, ilibainika kwamba ni mama mtarajiwa.


"Niliachana na ndoto zangu za kuwa mzazi, kisha mtoto huyu akatokea," alisema.


Kulingana na gazeti la New York Times, Schade alibainisha kuwa baba wa mtoto huyo aliamua kutojihusisha na maisha ya mtoto huyo, kwa kuwa bado hajajitokeza hadharani kama shoga.


"Hii haikuwa kile nilichotarajia, lakini ninaipenda familia yangu ndogo," Schade alisema.


Schade kisha alikutana na mume wake, Jordan Schade, 29, alipokuwa na ujauzito wa miezi mitatu, na akachukua majukumu kama baba.


Metro iliripoti kuwa kabla ya kupitia mabadiliko yake ya jinsia, alikuwa ametumia miaka akipambana na hisia kubwa ya kunaswa katika umbo lisilofaa.


Hata hivyo, alipokuwa mjamzito na kubeba binti yake kwa muda kamili, alikumbana na viwango vya kufadhaisha vya transphobia.


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad