Serikali Yashtakiwa Kwa Kusaini Makubaliano ya Bandari na Dubai


Serikali Yashtakiwa Kwa Kusaini Makubaliano ya Bandari na Dubai
Bandari


Waliofungua kesi hiyo ni Mawakili Emmanuel K. Changula, Alphonce Lusako, Raphael J. Ngonde na Frank J. Nyalusi wanaituhumu Serikali kupitisha mkataba huo kwa maelezo kuwa hauzingatii maslahi ya Nchi

Waziri wa Ujenzi na Katibu Mkuu wanashtakiwa kwa kusaini Makubaliano na kuyapeleka Bungeni bila kushirikisha Umma kutoa maoni ikiwa ni kinyume na Kifungu cha 11(1)(2) cha Sheria ya Rasilimali za Taifa No. 5 ya mwaka 2017

Aidha, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na Katibu wa Bunge wanashtakiwa kwa Kuliongoza Vibaya Bunge, Kupiga Kura ya Ndio ya Jumla badala ya Mbunge Mmoja Mmoja ambapo Washtakiwa wote wanatakiwa kufika Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya Julai 3, 2023

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad