Titan: Harakati Za Kutafuta Sababu Zilizochangia Nyambizi Kupasuka Zaanza

Titan: Harakati Za Kutafuta Sababu Zilizochangia Nyambizi Kupasuka Zaanza


Nahodha wa zamani wa manowari ya Royal Navy Ryan Ramsay ametaja baadhi ya sababu ambazo huenda zilipelekea nyambizi ya OceanGate ya Titan kupasuka kwenye mteremko wake kuelekea kulipotokea ajali ya Titanic.


Ramsay aliliambia shirika la habari la PA kwamba moja ya mambo mawili yanaweza kuwa yametokea – mwili wa nyambizi wenye nati 17 zilizotumika kuwafunga abiria ilishindwa kufanya kazi, jambo ambalo lilisababisha chombo hicho kupasuka “kwa sababu kuna shinikizo kubwa, hata tu kufika nusu ya chini ya bahari”.


Uwezekano mwingine ni kwamba huenda kulikuwa na kasoro ya awali katika mwili wa nyambizi yenyewe, na kusababisha matokeo kama hayo, aliongeza.


“Kitu chanya pekee ni kwamba ajali ilitokea mara moja na hata hawakujua kilichotokea,” alisema.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad