Utulivu wa Kocha Nabi na Uimara wa Uongozi Yanga Upewe Maua yake


Coach Nabi alisaini Yanga akitoka kufutwa kazi El Merreikh ya Sudan, akaja kufanya vyema akiwa Yanga yenye kikosi bora na Uongozi imara, ndipo nae ubora wake mkubwa ukadhihirika na akafanya makubwa sana.

Coach Nabi naamini anajitahidi sana kuwa mtulivu kabla ya kuchukua project yoyote mpya, jicho lake ni ubora wa kikosi, ukubwa wa project na Uongozi uliopo kwenye klabu husika.

Ni sahihi sana kumpa credit Coach Nabi kwa alichofanya Jangwani lakini nyuma yake yatupasa tukumbuke namna Uongozi ulimpa imaan ya kuonesha alichonacho.

Nani angesubiri kumtimua punde tu baada ya kuondelewa na Al Hilal ya Sudan kwenye Champions League? Nani angesubiri kumtimua kazi punde tu baada ya sare yao dhidi ya Club Africain nyumbani? Maana yake katikati kulikuwa na MUDA plus IMAAN.

Watu wengi ikiwemo Mashabiki wa Yanga walitaka Kocha afutwe kazi, lakini utulivu wa kuamini kwenye mchakato kutoka kwa Menejimenti ukaleta matunda makubwa ya Nabi ndani ya Yanga, thats Leadership.

Nje tu na ubora wa Makocha hizi timu zimewekeza sana na zinatupa gharama kubwa sana, katazame Bonus na gharama za uendeshaji wa hizi timu kama motisha achana tu na salaries.

Viongozi kukosolewa ni kawaida sana ila kunayo room ya kuwapongeza nyuma ya mafanikio ya Yanga, they had alot of smart moves.

VISIT MOROGORO🇹🇿

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad