Kusah Afunguka Tetesi za Kuachana na Aunty Ezekiel "Mimi Sasahivi ni Brand Siwezi Tena"


"Mimi na Aunty Ezekiel hatujaachana isipokuwa tumeacha kuongozana kila sehemu kama tulivyokuwa tunafanya huko nyuma, tumeacha kuongozana kwasababu kila mtu ana maisha yake na ndoto zake na kitu ambacho namwambia kila siku ni kuiheshimu kazi yangu na atambue mimi ni nani na yeye ni nani" amesema Kusah na kuongeza

"Leo hii haiwezekani sherehe kaalikwa Aunty tuende wote wakati mimi naijua thamani yangu imekuwa, hiyo time ambayo tulikuwa tunaenda wote nilikuwa sijajipata hata show nilikuwa nafanya bure lakini sasa hivi napewa hela kwenye kila show. Kwahiyo inakuwa ni ngumu kunikuta naye mara nyingi lakini tunapendana, tunaishi pamoja na hata chakula yeye ndiye ananiandalia"

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad