BREAKING: Rais Samia Afanya Uteuzi na Kutengua, Wakuu wa Wilaya


Rais Samia Afanya Uteuzi na Kutengua, Wakuu wa Wilaya

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo July 02, 2023 amefanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya ambapo ametengua uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Mwanahamisi Athumani Munkunda na kumteua Mobhare Holmes Matinyi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.

Rais Samia ametengua pia uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, Abel Yeji Busalama na amemhamisha kituo Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mjini, Hashim Shaib Mgandilwa kwenda kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilindi, pia amemteua James Wilbert Kaji kuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga.


Rais Samia Afanya Uteuzi na Kutengua, Wakuu wa Wilaya

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad