Robertinho: Nimeridhika na usajili wa wachezaji, benchi la ufundi

Robertinho: Nimeridhika na usajili wa wachezaji, benchi la ufundi


Kocha wa Simba SC, Roberto Oliviera 'Robertinho' amesema ameridhishwa na usajili wa kikosi pamoja na benchi jipya la ufundi lililosukwa kuelekea msimu wa mashindano 2023/24.


Robertinho amesema wachezaji wanaoendelea kusajiliwa pamoja na wale waliopo wanatengeneza kikosi imara ambacho anaamini kitawapa mataji msimu ujao.


Robertinho ameongeza kuwa kwa sasa kila nafasi ina wachezaji bora kuanzia wawili kitu ambacho kitakuwa msaada mkubwa msimu ujao.


"Nimeridhika na kikosi changu, wachezaji wapya waliosajiliwa ni wazuri hata wale waliopo wako imara. Tunaamini maandalizi yetu yatakuwa mazuri nchini Uturuki.


"Kuna wachezaji wengine wapya tutaungana nao tukiwa Uturuki kukamilisha kikosi. Msimu ujao tunahitaji kucheza vizuri na kushinda mataji, Simba ni timu kubwa na hilo lipo ndani ya uwezo wetu," alisema Robertinho.


Kuhusu benchi jipya la ufundi, Robertinho amesema;


"Makocha wote walioletwa wana wasifu mzuri, wana vigezo vyote vilivyoidhinishwa na Mamlaka naamini tutafanya vizuri."

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad