Tanzania Kuna Watu 600 Wanasubiria Kunyongwa, Adhabu Hii Iondolewe, Wajirekebishe : Chande



Jaji Mkuu Mstaafu, Mohamed Chande ametoa ripoti ya Tume ya Haki na Jinai huku akitoa mapendekezo mbalimbali kama vile adhabu ya kunyongwa iondolewe ama mtu akiua hukumu isiwe tu kunyongwa hadi kufa bali kuwepo na adhabu ingine.

‘Yapo maoni na malalamiko kwamba kifungo cha maisha kiwape nafasi wafungwa nafasi ya kujirekebisha na kulitumikia taifa na kwamba wakati umefika kifungo hiki kiwe na ukomo ili kuwawezesha wafungwa wanaotumikia kifungo cha maisha kuwa na matumaini’amesema Jaji mstaafu.

Aidha ameweka wazi kuwa kuna watu Zaidi ya 600 wanaosubili kunyongwa na hata hivyo wengi wao wanaishi na hofu kubwa kwani wana miaka kadhaa wakingoja adhabu hiyo.

Jaji Mkuu Mstaafu, Mohamed Chande ameyasema hayo alipokuwa akiwakilisha ripoti ya Tume ya Haki Jinai.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad