Ikulu ya Urusi Yakanusha Vikali Kumuua Mkuu wa kundi la Mamluki la Wagner


Ikulu ya Urusi (Kremlin) imekanusha vikali kuhusika kwa namna yoyote na ajali ya ndege inayosemekana kumuua Mkuu wa kundi la mamluki la Wagner, Yevgeny Prigozhin, ikisema tuhuma hizo ni uzushi usiokuwa na maana.

Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Dmitry Peskov, amesema shutuma dhidi ya Nchi yake hazina mashiko yoyote na badala yake ametizupia lawama nchi za Magharibi kwa kusambaza uvumi usio maana.

"Tazama, kwa sasa kuna uvumi mwingi sana kuhusiana na ajali hii ya ndege na vifo vya abiria wa ndege hiyo akiwemo Yevgeny Prigozhin, bila shaka, katika Nchi za Magharibi, uvumi huo unawekwa kwa njia fulani na wote ni uongo mtupu na bila shaka ni muhimu kutumia ukweli unaporipoti kuhusiana na suala hili, kwa sasa ukweli ni mchache kwa sababu uchunguzi bado unaendelea”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad