Kikosi cha Yanga vs KMC Leo 23/8/2023

 
Kikosi cha Yanga vs KMC Leo 23/8/2023



Kikosi cha Yanga vs KMC Leo 23/8/2023

Yanga ambayo imeonyesha mpira wa kasi kwenye mechi tatu zilizopita, imekuwa maridadi pia katika gongagonga na kushambulia kupitia pembeni. Lakini KMC mpya ya Abdihamid Moallin imekuwa ikicheza soka la kuvutia na ina mabadiliko makubwa ya kiuchezaji ikianza na mechi iliyopita dhidi ya Namungo ugenini ilikolazimisha sare.

Yanga ambao ni mabingwa wa ligi mara 29, inaingia katika mchezo huu ikiwa na rekodi ya kulichukua taji hilo mara mbili mfululizo, huku mashabiki wake tangu juzi kwenye mitandao ya kijamii ya klabu hiyo wakikomenti kwa wingi wakimshinikiza Gamondi kumwanzisha Straika Mghana, Hafiz Konkoni ili wajue kama yaliyomo yamo tofauti na sasa anavyomchezesha dakika zisizozidi 10.

Timu hizi zinakutana huku zote zikiwa na makocha wapya na Yanga inaongozwa na Muargentina, Gamondi aliyechukua nafasi ya Nabi huku kwa KMC ikiongozwa na kocha wa zamani wa Azam FC, Moallin.

🏆 NBC Premier League

⚽️ Young Africans SC Vs KMC FC

📆 23.08.2023

🏟 Azam Complex, Chamazi

🕖 1:00 Usiku


 
Kikosi cha Yanga vs KMC Leo 23/8/2023

  • Metacha 
  • Yao
  • Kibabage
  • Job
  • Bacca
  • Aucho
  • Moloko
  • Mudathir
  • Musonda
  • Pacome
  • Aziz K

 

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad