Mkude Aagwa Simba Day Licha ya Kutoonekana Uwanjani


Mkude Aagwa Simba Day Licha ya Kutoonekana Uwanjani

Kiungo aliyeitumikia Simba kwa miaka 13 Jonas Mkude ameagwa kwa kupigiwa makofi kwenye tamasha la Simba Day.

Mkude sasa anakipiga Yanga baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja wa kuitumikia timu hiyo yenye maskani yake Jangwani.

Mkude ametupiwa vilago na Simba dirisha hili la usajili baada ya mkataba wake kumalizika na jezi yake namba 20 aliyokuwa akiivaa alipokuwa Simba amekabidhiwa beki wa kati wa kimataifa Che Malone.

Pamoja na kutokuwepo kwenye tamasha hilo kutokana na kuwa kambini kwenye timu yake mpya mashabiki wa Simba waliombwa kusimama na kumpigia makofi kutokana na kuitumikia timu hiyo kwa muda mrefu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad