Soka la Kocha Mpya Gamondi Lawakosha Maboss Yanga


Mabosi wa Yanga wameumizwa na kitu kimoja tu juzi, kupoteza taji la Ngao ya Jamii ambalo walilishikilia kwa misimu miwili, lakini kuna kauli ya mamlaka wakaitoa juu ya kikosi chao. Kauli hiyo ilitolewa na Makamu wa Rais wa timu hiyo, Arafat Haji akisema licha ya kupoteza taji hilo, lakini wako timamu wakiwa na matumaini na soka la kocha mpya, Miguel Gamondi.

“Tumeumia kupoteza hii Ngao, lakini kiukweli tuna matumaini makubwa na timu yetu. Tungefungwa ndani ya dakika 90 tungesema kuna shida mahali, lakini sote tunafahamu penalti hazina mwenyewe,”

“Timu yetu imecheza mpira mkubwa. Tunajua (Simba) wanashangilia kuchukua Ngao, lakini kwenye mioyo yao wanajua ni namna gani waliteseka kwenye mchezo ule. Viongozi wao tulikuwa nao pale juu (jukwaani Uwanja wa Mkwakwani) tuliwaona. Tunajivunia sana wachezaji na makocha wetu.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad