Haitham Kim Kuzikwa Kesho

Haitham Kim Kuzikwa Kesho

Haitham Kim Kuzikwa Kesho

Msanii wa Bongo fleva, Haitham Ghazal Seif 'Haitham Kim' atazikwa kesho katika Makaburi ya kisutu Dar es Salaam.


Msanii huyo amefariki leo ijumaa majira ya saa 6 mchana katika hospitali ya Temeke iliyopo jijini Dar es Salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.


BNB ambaye ni rafiki wa Mume wa marehemu amesema kuwa Haitham alikuwa akisumbuliwa na mapafu na kushindwa kupumua hadi umauti ulipomkuta.


Haitham ameacha mume wake Bryson na watoto wawili.


Ikumbukwe Baadhi ya nyimbo na wasanii aliowahi kufanya nao kazi ni pamoja na ngoma ya Utamu na Young Lunya nyingine ni Utaniumiza Dayoo na Lody Music.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad