Ajali ya Wanafunzi, Mwalimu Asimamishwa Kazi

 

Ajali ya Wanafunzi, Mwalimu Asimamishwa Kazi

Mwalimu Furaha Msule anayefundisha Shule ya Sekondari Kidegembye iliyopo Lupembe Halmashauri ya Wilaya ya Njombe amesimamishwa kazi kwa kosa la kuwachukua Wanafunzi na kuwapeleka kupakia kuni zake kinyume na sheria na kupelekea kupata ajali ya gari wakati wakirudi majira ya saa moja usiku.


Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Christopher Sanga amethibitisha kusimamishwa kazi kwa Mwalimu Msule na kutoa wito kwa Watumishi kufanya kazi kwa kufuata sheria kanuni na taratibu.


"Ofisi ya Mkurugenzi kwa kushirikiana na Tume ya Walimu imechukua hatua ya kumsimamisha kazi Mwalimu aliyehusika huku utaratibu, sheria na kanuni nyingine zikiendelea"


Sanga amesema October 01,2023 ofisi yake ilipokea taarifa ya kutokea kwa ajali ambapo Mwalimu Furaha aliwachukua Wanafunzi na kwenda kupakia kuni zake lakini kwa sasa Wanafunzi wote 11 wakiwemo 6 waliokuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Kibena wameruhusiwa na kurejea Shuleni.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad