Feisal Salum Fei Toto Kutua Simba Sports Club, Ataka Afrika Nzima Imjue



Kiungo mshambuliaji wa Azam Fc FEISAL SALUM ABDALLAH FEI TOTO hana furaha ndani ya klabu ya Azam na chanzo cha karibu cha mchezaji huyo kimenithibithia kuwa mchezaji huyo anataka kucheza Simba Sports Club msimu ujao timu kongwe kubwa na bora ukanda huu wa CECAFA.

Chanzo hicho kinasema malengo yake ni kujibrand Africa nzima imjue na hawezi kufikia malengo hayo kama ataendelea kubakia kucheza Azam Fc timu ambayo haiwezi kuchukua ubingwa wa ligi kuu au kumaliza nafasi ya pili ili ipate tiketi ya kucheza Ligi ya Mabingwa Barani Africa CAF CHAMPIONS LEAGUE.

Feisal Salum Abdallah Fei Toto anasema timu pekee itakayofanya aonekane Africa nzima na afike mbali kimataifa ni Simba Sports Club pekee kwa sasa ndio anaiona timu yenye malengo makubwa ya kuliteka soka la Africa yeye kama kijana mdogo mwenye ndoto za kufika mbali anatamani sana kucheza Simba Sports Club atafanya kila linalowezekana ili atue kwenye klabu hiyo ambayo itatimiza ndoto zake kwa vitendo na sio maneno.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad