Hivi Ndivyo Timu ya Ihefu Walivyotumia Umafia na Kuifunga Yanga Mbili Kwa Moja


Kikosi cha Yanga SC kimeendeleza uteja wake dhidi ya Ihefu baada ya kukubali kichapo cha 2-1 katika Uwanja wa Highland mkoani Mbeya .
Ni mabao ya Lenny Kissu dakika ya 40 na lile la ushindi likifungwa na Charles Ilanfya dakika ya 67.

Bao la Yanga limefungwa na Pacome Zouzoua dakika ya 3 ikiwa ni bao la mapema Uwanja wa Highland Estate.

Wachezaji wa Ihefu walikuwa wakipoteza muda hovyo kwa kujiangusha huku Ilanfya akiwa kiongozi wao na alionyeshwa Kadi dakika ya 90 ya njano.

Watoa huduma ya kwanza nao mwendo wa kinyonga katika kutoa huduma ya kwanza ilikuwa ni taratibu Sana sio Sawa, Benchi la ufundi kwa timu zote hakukuwa na utulivu.

Ikumbukwe kwamba dakika 45 za mwanzo kilatimu ilionyesha ushindani mkubwa huku timu zikicheza kwa kushambuliana.

Mashabiki wa Yanga nao kipindi cha pili walionekana wakifanya kitendo cha hovyo kwa kurusha chupa uwanjani jambo ambalo sio sawa.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad