Jonas Mkude Amfungulia Mashtaka MO DEWJI Adai Fidia ya Mamilioni ya Pesa

 

Jonas Mkude Amfungulia Mashtaka MO DEWJI Adai Fidia ya Mamilioni ya Pesa

Mchezaji wa Klabu ya Yanga, Jonas Mkude amefungua kesi katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam akiidai Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (METL) fidia ya Sh 1 bilioni kwa kutumia picha zake katika mitandao mbalimbali ya kijamii ikiwemo Instagram na Twitter bila idhini yake.

Mkude amefungua kesi ya madai 192 ya mwaka 2023 mbele ya Jaji Butamo Philip dhidi ya kampuni hiyo akiidai fidia hiyo Kwa kuvunja haki yake ya msingi.

Mkude amejiunga na Yanga msimu huu akitokea Simba aliyotumikia kwa misimu 12.

Kampuni ya Mohamed Enterprises Tanzania Limited (METL) yako chini ya Rais wa Heshima wa Simba Mohammed Dewji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad