Mbinu Walizotumia Kundi la Hamas Kuivamia Israel

 

Mbinu Walizotumia Kundi la Hamas Kuivamia Israel

Waisraeli wengi huenda walikuwa wamelala ilipoanza.


Jumamosi ilikuwa Sabato ya Kiyahudi na pia sikukuu takatifu, kumaanisha kwamba familia zilikuwa zikipanga kutumia wakati nyumbani pamoja au katika sinagogi, na marafiki walikuwa wakikutana.


Lakini kutoka angani alfajiri, mvua ya mawe ya roketi iliashiria kuanza kwa shambulio ambalo halijawahi kutokea katika kiwango kile.


Kwa miaka mingi, Israel imeimarisha kizuizi kati yake na eneo dogo la Wapalestina la Gaza. Ndani ya saa chache, kutopitika kwake kulifichuliwa kuwa na kasoro.


Karibu 06:30 saa za ndani, roketi zilianza kuruka.


Kundi la wapiganaji wa Kiislamu, linalodhibiti Gaza na kuorodheshwa kuwa kundi la kigaidi nchini Uingereza na kwingineko duniani hutumia mbinu hii mara kwa mara.


Makombora hayo ya kizamani mara nyingi yanatatizika kukwepa mfumo wa hali ya juu wa ulinzi wa makombora wa Iron Dome wa Israeli, lakini maelfu yalirushwa katika muda mfupi ili kuushinda.


Kiwango kinaashiria kuwa kulikuwa na miezi ya kupanga hilo.


Hamas inasema ilifyatua 5,000 katika duru ya kwanza (Israel inasema ilikuwa nusu ya idadi hiyo).


Ving’ora vya mashambulizi ya anga vilianza kusikika hadi Tel Aviv – kilomita 60 kutoka Gaza na Yerusalemu ya magharibi na moshi ulionekana ukipanda juu ya miji ambayo kulikuwa na milio ya moja kwa moja.


Wakati roketi hizo zikiendelea kurushwa, wapiganaji walikuwa wakikusanyika ambapo walipanga kupenya kizuizi kikubwa cha Gaza.


Ingawa Israel iliondoa wanajeshi wake na walowezi kutoka Gaza mwaka 2005, bado inadhibiti anga yake, mpaka wa pamoja na ufuo.


Pamoja na doria za kawaida za kijeshi kuzunguka eneo hilo ambalo ni ukuta wa zege katika baadhi ya maeneo na uzio katika maeneo mengine, pia kuna mtandao wa kamera na vihisi ili kuzuia uvamizi.


Lakini ndani ya saa chache, kizuizi kilikuwa kimevunjwa tena na tena.


Baadhi ya wapiganaji wa Hamas walijaribu kukwepa kizuizi kabisa, ikiwa ni pamoja na kuruka juu yake kwenye paraglider (picha ambazo hazijathibitishwa zilionesha angalau saba zikipeperushwa juu ya Israeli) na kwa mashua.


Vikosi vya Ulinzi vya Israel vimesema vimezuia majaribio mawili ya Hamas ya kuvuka kuingia Israel kwa kuifikisha meli ufukweni.


Lakini kinachotenganisha shambulio hili ni mashambulizi kadhaa yaliyoratibiwa, ya moja kwa moja kwenye maeneo ya vizuizi.


Saa 05:50 kwa saa za huko, akaunti ya Telegram inayohusishwa na mrengo wenye silaha wa Hamas ilichapisha picha za kwanza kutoka ardhini, zilizopigwa Kerem Shalom, kusini zaidi mwa vivuko vya Gaza.


Walionesha wanamgambo wakivuka kizuizi na miili iliyojaa damu ya wanajeshi wawili wa Israel ikiwa chini.


Picha nyingine ilionesha pikipiki zisizopungua tano, kila moja ikiwa na wanamgambo wawili waliokuwa na bunduki, zikipita kwenye shimo lililokuwa limekatwa kwenye sehemu ya uzio wa waya wa kizuizi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad