Baada ya Machungu ya Bao Tano Kupoa, Simba Waanza Mazoezi Rasmi ya Klabu Bingwa

 

Baada ya Machungu ya Bao Tano Kupoa, Simba Waanza Mazoezi Rasmi ya Klabu Bingwa

Wekundu wa Msimbazi Simba SC, leo Novemba 13, 2023 wamerejea kwenye mazoezi ya kujiandaa na mechi za Klabu Bingwa.


Wachezaji wa Simba walipewa muda wa kupumzika mwishoni mwa wiki iliyopita baada kukamilisha mchezo wao dhidi ya Namungo FC na ratiba ya Timu za Taifa kuingia.


Akizungumza na Wasafi FM, Ahmed Ally ambaye ni meneja wa habari na mawasiliano wa klabu hiyo, amesema wachezaji wao wote wamerejea kambini leo baada ya kuwapa mapumziko ya takriban siku 3.


"Wachezaji wote wanarejea kwenye mazoezi, hakuna mchezaji hata mmoja aliyesimamishwa, tunarudi mazoezini," alisema Ahmed.


Simba wanajiandaa na michezo ya Klabu Bingwa hatua ya makundi inayotarajiwa kuanza Novemba 25, 2023 ambapo Simba ataanzia nyumbani dhidi ya ASEC Mimosas.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad