Kanye West Hamnazo Kabisa, Ahamisha Makazi yake Jangwani Huko Saudi Arabia

Kanye West Hamnazo Kabisa, Ahamisha Makazi yake Jangwani Huko Saudi Arabia

Kanye West Hamnazo Kabisa, Ahamisha Makazi yake Jangwani Huko Saudi Arabia



Kanye West alichagua utulivu, na kuhamishia makazi yake Jangwani huko nchini Saudi Arabia ambako alipiga kambi ya muda mfupi kwa ajili ya kukamilisha albamu yao ijayo ambayo ilitakiwa kutoka mwezi Oktoba.

Mpangilio wa kambi hiyo ya Jangwani , ulijumuisha studio ya kurekodi na bwawa la kuogelea katikati ya miamba, ambapo kambi hii ilikuwa kwa ajili ya kukamilisha albamu ya pamoja na Ty Dolla $ign, ambayo inatarajiwa kutoka kabla ya mwisho wa mwaka huu.



Licha ya kucheleweshwa mara kadhaa, Ty Dolla $ign ameahidi mashabiki kwamba albamu yao inakuja hivi karibuni, "Coming Real Soon". Alitoa habari hizi wakati wa show yake, kwamba amerejea kutoka safari ya Saudi Arabia ambapo alifanya kazi zaidi kwa ajili ya ujio wao.

Ye amekuwa na utaratibu wa kutafuta maeneo ya kipekee kwa ajili ya kuandaa kazi zake, huku mwaka 2018 aliweka kambi nchini Uganda ambako alipata nafasi ya kukutana na Yoweri Museveni, Rais wa nchi hiyo.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad