Kisasi Cha 5G Kulipwa, TFF Wazikutanisha Tena Simba na Yanga Hivi Karibuni

Kisasi Cha 5G Kulipwa, TFF Wazikutanisha Tena Simba na Yanga Hivi Karibuni


Kikosi cha timu ya wanawake cha Yanga, Yanga Princess kinatarajiwa kucheza dhidi ya Simba Queens katika mchezo wa Ngao ya Jamii Wanawake hatua ya nusu fainali.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Yanga Princess itapambana na Simba Queens Desemba 9, mwaka huu kwenye Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam.

Mshindi wa mechi hiyo atacheza fainali dhidi ya mshindi wa nusu fainali nyingine kati ya JKT Queens na Fountain Gate Princess.

Mechi hizo za Ngao ya Jamii, ni ishara ya ufunguzi wa msimu mpya wa Ligi Kuu ya Wanawake 2023-2024.

Fainali ya Ngao ya Jamii Wanawake itachezwa Desemba 12, 2023, kabla ya mchezo huo wa fainali, mapema itapigwa ya kumsaka mshindi wa tatu. Mechi zote hizo zitachezwa Uwanja wa Azam Complex.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad