Ally Kamwe: Mechi ya Medeama haitakuwa rahisi

Ally Kamwe: Mechi ya Medeama haitakuwa rahisi


Klabu ya Young Africans imesafiri kuelekea nchini Ghana alfajiri ya leo kwa ajili ya mchezo wa tatu wa hatua ya makundi ya Ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Medeama.


Afisa habari wa klabu hiyo Ali Kamwe amesema wanatarajia kukutana na upinzani mgumu katika mchezo huo na hautakuwa mchezo rahisi.


Ali Kamwe amewaomba wadau na mashabiki wa soka nchini kuiombea timu yao na panapo majaaliwa watarejea na ushindi nchini.


Yanga ipo mkiani mwa kundi D ikiwa na alama moja pekee katika michezo miwili iliyocheza.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad