Azam FC Kuongoza Ligi Kuu Leo KMC Wakikubali Unyonge


Azam FC
Azam FC


AZAM FC ipo moto, KMC wapo vizuri na leo usiku zinakutana kwa mara ya kwanza msimu huu katika mechi ya Ligi Kuu. Timu hizo zinakutana kuanzia saa 3 usiku, baada ya Bodi ya Ligi kuurudisha nyuma mchezo huo ambao awali ratiba ilionyesha ungepigwa kesho Ijumaa, huku kila moja ikiwa na kiu ya kusaka pointi tatu ili kuziweka pazuri kwenye msimamo.

Azam ipo nafasi ya pili ikiwa na pointi 22 baada ya mechi 10, ikifunga mabao 24 na kufungwa tisa, huku KMC ikishika nafasi ya tano ikiwa na pointi 19, ikifunga mabao 13 na kufungwa mabao 14.

Kama Azam itashinda mchezo huo itapaa hadi KILELENI ikiing’oa Yanga yenye alama 24 kwa sasa, kwani Wana lambalamba hao watafikisha 25, lakini ikilazimishwa sare inaweza kuongeza pengo la pointi kati yao na Simba ilipo nafasi ya tatu na pointi 19 kama ilizonazo KMC. Kwa namna timu hizo zilivyo na ushindani uliopo ni wazi haitakuwa mechi nyepesi.

Unadhani nani ataibuka mbabe leo ..!!👇

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad