Huu Hapa Ukweli Usiosemwa Kuhusu Kufungwa Kwa SIMBA Jana

 

Huu Hapa Ukweli Usiosemwa Kuhusu Kufungwa Kwa SIMBA Jana

KLABU ya Mlandege Fc imefanikiwa kuutetea ubingwa wake mara baada ya kuichapa Simba Sc bao 1-0 kwenye fainali ya michuano ya Mapinduzi Cup ambayo ilikuwa inaendelea visiwani Zanzibar.

Katika mchezo huo ambao Simba Sc ilifanikiwa kuutawala mchezo kwenye vipindi vyote licha ya kutofanikiwa kupata bao huku wakiruhusu kufungwa bao moja na kushindwa kunyakua taji hilo.

Bao pekee ambalo limewafanya Mlandege Fc kuibuka washindi limefungwa na Joseph Akandwanao mnamo dakika ya 54 ya mchezo baada ya kuwatoka mabeki wa Simba Sc na kupiga shuti kali lililomshinda kipa na kuingia nyavuni.

Hata hivyo, Joseph alikuwa kama sapraizi kwa upande wa Simba kwa kuwa kwenye michezo mingine ya nyuma hakuwahi kuonekana kama ambavyo jana Simba ilimtumia, Ladack Chasambi.

Mwaka jana, Mlandege ilitwaa ubingwa huu baada ya kuichapa Singida mabao 2-1 na imeweka rekodi ya kuwa timu ya Zanzibar kutwaa ubingwa huo mara mbili.

Hii ilikuwa mechi ya kwanza kwa Mlandege kushinda ndani ya dakika tisini kwenye michuano hii msimu huu baada ya michezo yake yote kutoka sare na mingine kuingia kwa mikwaju ya penalti.

Katika mchezo wa jana, Simba ilikosa nafasi kadhaa kupitia kwa Fabrice Ngoma, Willy Esomba Onana na Jean Baleke huku, Mlandege ikianza kwa kukosa nafasi ya wazi dakika ya 17 baada ya kipa Ayoub Lakred kufanya makosa lakini ikashindwa kuitumia nafasi hiyo.

USHAMBULIAJI TATIZO SIMBA

Simba bado inatakiwa kuendelea kutafuta dawa ya safu ya ushambuliaji ambayo licha ya Kocha Abdelhak Benchikha kuwatumia washambuliaji wake wawili vinara Mosses Phiri na Jean Baleke wote wakicheza kipindi kimoja bado hawakuwa na kitu cha kuisaidia timu hiyo.

“Hayakuwa matarajio yetu, lakini tuseme ndiyo mpira ulivyo, tunawaomba mashabiki waendelee kutuunga mkono,” nahodha wa Simba Shomary Kapombe alisema.

ALIKIBA NDANI

Msanii Alikiba ndiye aliyekuwa msanii mkubwa aliyenogesha burudani kwenye mchezo huo huku wimbo wake wa Mnyama maalumu kwa Simba, ukiteka umati wa mashabiki wengi wa Simba wakiuimba Uwanja mzima.

RAIS KAMA KAWA

Rais wa Zanzibar Hussein Mwinyi kama kawaida ndiye aliyekuwa mgeni rasmi kwenye mchezo huo akitinga mapema tu dakika 25 kabla ya mchezo kuanza pia akiwemo makamu wake wa pili Hemed Suleiman na viongozi wengine wa serikali kwa Bara na Zanzibar.

TUZO

Mchezaji bora wa Mashindano: Fabice Ngoma (Simba) Kipa Bora wa Athuman Hassan (Mlandege). Mfungaji Bora: Elvis Rupia Singida Fountain Gate

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad