KUMEKUCHA: Tanzania Yafuta Vibali vya Ndege ya Kenya Airways Kufanya Safari Nairobi Dar es Salaam


Taarifa ya Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania imeeleza kuwa kwa niaba ya Mamlaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, imeamua kufuta vibali vya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) vya kuendesha safari za abiria kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia 22 Januari 2024

Taarifa hiyo imedai hatua hii ni baada ya uamuzi wa Mamlaka ya Anga ya Jamhuri ya Kenya kwenda kinyume na Kifungu cha 4 cha Mkataba wa Maelewano kuhusu Huduma za Ndege, kati ya Tanzania na Kenya yaliyotiwa saini Novemba 24, 2016 Jijini Nairobi

Kufuatia uamuzi huu, hakutakuwa na safari za ndege za abiria kwa KQ kati ya Nairobi na Dar es Salaam kuanzia tarehe 22 Januari 2024

Jamii Forums
Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad