SGR Isipoanza Kazi 2024 CCM Itakula Vichwa - PAUL Makonda

 

SGR Isipoanza Kazi 2024 CCM Itakula Vichwa - PAUL Makonda

Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo Paul Makonda, leo Januari 19,2024 ameanza ziara yake kwa kuongea na Wakazi wa Tegeta Jijini Dar es salaam ambapo pamoja na mambo mengine amesema Waziri wa Uchukuzi Prof. Makame Mbarawa na Mkurugenzi wa TRC, Masanja Kadogosa wameahidi kuwa mwaka huu treni za mwendokasi zitaanza safari kutoka Dar es salaam hadi Dodoma ambapo amesema wasipofanya hivyo CCM itakula vichwa.


Makonda amenukuliwa akisema:


“Tulimuita Waziri wa Mbarawa na Kadogosa ya kwamba kumekuwepo na mabadiliko ya tarehe ya kuanza kwa treni ya mwendokasi napo majibu yametoka na mwaka huu kama kuna ahadi nyingine zaidi ya kuiona treni inatoka Dar es salaam kwenda Dodoma wakatupa ahadi CCM inakula vichwa, muda wa ahadi umeisha.”

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad