Harmonize Asitisha Tamasha la Sierra Leone Baada ya Mpenzi Wake Kunyimwa visa




Harmonize asitisha tamasha la Sierra Leone baada ya mpenziwe kunyimwa visa

Harmonize na barafu ya moyo wake, Poshy Queen.
Mwanamuziki wa Tanzania Harmonize ameamua kusitisha tamasha lake la Sierra Leone baada ya mpenzi wake kunyimwa Visa ya kuingia nchini humo.

Kupitia instastori yake siku ya Jumapili, Konde Boy aliwaomba radhi mashabiki wake nchini Sierra Leone akisema hatafanikiwa kufika huko.

"Sierra Leone, sitafika tarehe 14/02 samahani. Tuonane wakati mwingine. Baadhi ya wanachama wa genge walikosa visa akiwemo mpenzi wangu. Kama unavyojua ni valentine, siku ya kipekee sana. Siwezi kuruka bila yeye. Tarehe mpya hivi karibuni," mwanamuziki huyo alisema.

Harmonize na Poshy Queen waliweka hadharani uhusiano wao baada ya wiki kadhaa za uvumi.

Mnamo Januari 15, mtunzi huyo wa kibao I'm Single alitumia mitandao yake ya kijamii kukiri mapenzi yake kwa Poshy Queen.


Konde Boy alisema kuwa tayari amempa Poshy Queen nywila zake zote za mitandao ya kijamii na wale wanaoingia kwenye DM zake wanapaswa kuwa makini.

"Mtu mwaminifu duniani. Mapenzi yangu huenda na simu yangu ya rununu, tayari ana nywila ya simu yangu. Iwapo utapata jibu la kushangaza bado nina upendo kwa ninyi nyote, "alisema.

Mwanamuziki huyo wa Tanzania alisema;

"Tulipanga kuungana hapo awali lakini haikuwezekana. Nakutakia kila la kheri hapa ndio mwisho wangu. Onyoo. Hajawahi tembea na yeyote ninae mjua. Heshimu hapa kama msichana wangu. Popote utakapomuona. Acha Drama."


Posh kwa upande wake aliweka picha ya Harmonize na nukuu inayosema "Adam wangu mimi hapa."

Poshy Queen ni mwanasosholaiti wa Tanzania na mfanyabiashara.

Hapo awali, Harmonize aliwahi kutoka kimapenzi na Poshy Queen, lakini uhusiano wao uliisha kwa uchungu.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad