Papa Afunguka 'Wanaokosoa Baraka Kwa Wapenzi wa Jinsia Moja Niwanafiki'



"Hakuna mtu atanipa kashfa ikiwa nitatoa baraka zangu kwa mfanyabiashara anayewanyonya watu, na hii ni dhambi kubwa sana. Lakini nitapewa kashfa ikiwa nitatoa kwa wapenzi wa jinsia moja, Huu ni unafiki"

Papa Francis amesema anaona kuna "unafiki" katika kukosolewa kwa uamuzi wake wa kuruhusu makasisi kuwabariki wapenzi wa jinsia moja.

Baraka za wapenzi wa jinsia moja ziliidhinishwa mwezi uliopita na hati ya Vatican iitwayo Fiducia Supplicans (Supplicating Trust), lakini ulikumbana na upinzani mkubwa katika Kanisa Katoliki, hasa kutoka kwa maaskofu wa Afrika.

Francis aliliambia jarida la Kikatoliki la Italia Credere kuwa "daima" anawakaribisha wapenzi wa jinsia moja na waliooana tena baada ya talaka kwenye sakramenti ya kuungama.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad