Rais Samia Aipongeza Yanga kwa Kutinga Robo Fainali ya CAFCL, Walamba Milioni 20

Rais Samia Aipongeza Yanga kwa Kutinga Robo Fainali ya CAFCL, Walamba Milioni 20


Rais was Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameipongeza Klabu ya Yanga kwa kufanya vizuri katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) baada ya kuifunga CR Belouizdad bao nne kwa sifuri na kufanikiwa kufuzu hatua ya Robo Fainali, akisema mafanikio hayo yameandika historia kubwa kwa klabu na sekta ya michezo nchini.


Rais Samia amenukuliwa akisema; “Naipongeza Klabu ya Yanga kwa kufanya vyema katika hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF), na kufanikiwa kufuzu hatua ya Robo Fainali. Mafanikio haya yameandika historia kubwa kwa klabu na sekta ya michezo nchini. Mmeleta furaha kwa mamilioni ya mashabiki wenu na Watanzania kwa ujumla.”

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad