Tajiri GSM Kujenga Uwanja wa Yanga Jangwani

Tajiri GSM Kujenga Uwanja wa Yanga Jangwani


Rais wa Yanga Eng. Hersi Said katika kuadhimisha miaka 89 ya Klabu ya Yanga ametangaza rasmi kuwa Mfadhili wa Timu hiyo Ghalib Said Mohammed (GSM) amekubali kujenga uwanja wa Yanga katika eneo la Jangwani.


“Baada ya mazungumzo ya muda mrefu na Mdhamini na Mfadhili wa Klabu yetu, Ghalib Said Mohammed (GSM), nipende kuwataarifu Wanachama na Mashabiki wa Klabu yetu kuwa leo, GSM ameridhia kwa dhati kushiriki kwenye kufanikisha ujenzi wa uwanja wa kisasa wa Young Africans Sports Club, katika eneo la Makao Makuu ya Klabu yetu, Jangwani, Jijini Dar Es Salaam.


“Nichukue fursa hii kumshukuru sana GSM kwa dhamira hiyo inayokwenda kutimiza ndoto ya Uongozi wangu, Kamati ya Utendaji na Wanachama na Mashabiki wa Young Africans kwa kuwa na uwanja wetu”

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad