Yanga Kapigwa Huko, Hakika Jina la Kipre Cheche Limeingia Katika Vitabu vya Gamondi



Mechi imemalizika kwa Mkapa na Azam wameibuka kidedea baada ya kuwatandika wananchi 2-1 Shuurani kwa Sillah na Fei Toto ambao wameitakatisha Azam huku bao ka kufutia machozi la Yanga likifungwa na Mzize.

Leo Wananchi wataliota jina la Kipre Jr hakika huyu kijana alikuwa mwiba mkali kwa Yanga.

Kama kawaida azam wakiwa na mpira walikuwa kwenye shape ya 4-2-3-1 huku kati kati ya uwanja wakijaza viungo watatu (Yahya Zayd,Bitegeko na Fei Toto) kisha Kipre alisimama mbele kama “false nine”

kwanini Kipre kakivuruga kiungo cha Yanga?

Mikimbio ya Kipre ilikuwa hatari kwa kiungo cha Yanga kwani Azam wakianza kujenga mashambulizi kijana alitoka kwenye box la Yanga na kushuka chini kwenye Midfield na kutengeneza idadi ya viungo wanne “Midfield Box” dhidi ya viungo watatu wa Yanga,Kisha Dickison Job alitoka kwenye eneo lake la nyuma na kujaribu kumfuata Kipre,kitu ambacho kilisababisha Ibrahim Bacca kubaki nyuma peke yake…..na kamwe hakuweza kupambana na mawinga wa Azam.

All in All Yanga leo hawakuwa na siku nzuri kwani wachezaji wao muhimu waliumia,pili Sub ya Guede haukuwa sahihi nadhani muda ule alitakiwa kuingia Okrah ili kuongeza kasi,tatu Yanga hawakucheza kwa intensity kabisa.

Halafu yule Manyama apewe ulinzi jamaa anajua kuzuia🔥

FT Azam 2-1 Yanga.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad