Yanga Wapewa Mamelodi Sundowns Robo Fainali CAF

 

Yanga Wapewa Mamelodi Sundowns Robo Fainali CAF

Hayawi hayawi sasa yamekuwa. Klabu ya Yanga imepangwa na Timu ya Mamelodi Sundowns kutoka Afrika ya Kusini hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Yanga walikuwa na nafasi ya kukutana na wapinzani watatu ambao ni Asec Mimosas, Mamelodi Sundowns na Petro Atletico De Luanda na bahati ikaangukia kwa wajukuu wa Nelson Mandela.

Michezo ya mzunguko wa Kwanza itapigwa kati ya Machi 29-30 Uwanja wa Mkapa na mchezo wa mzunguko wa pili utapigwa kati ya April 5-6 Afrika ya Kusini.

Je Unadhani Yanga wana nafasi ya kutoboa nusu Fainali mbele ya Mamelodi? Tupe maoni yako


Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad