13 Wafariki Dunia Ajalini Kilwa, Sita Wajeruhiwa

 

13 Wafariki Dunia Ajalini Kilwa, Sita Wajeruhiwa

Watu 13 wamefariki dunia na wengine sita kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari mawili eneo la Somanga wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi.


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi, John Imori amesema leo Jumatatu Aprili 22 ,2024 kuwa, ajali hiyo iliyotokea saa mbili asubuhi Barabara Kuu ya Somanga-Nangurukuru baada ya gari ndogo ya abiria kugongana uso kwa uso na lori la mafuta


Majeruhi wote sita wamepelekwa katika Hosptali ya Tingi kwa ajili ya matibabu zaidi pamoja na miili 13 imehifadhiwa kwenye chumba cha kuhifadhia maiti cha Hosptali ya Tingi iliyopo wilayani Kilwa, mkoani Lindi.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad