Ahmed Ally : Wanasimba Tuvumilie Kupita Kwenye MOTO Huu Mkali....

 

Ahmed Ally : Wanasimba Tuvumilie Kupita Kwenye MOTO Huu Mkali....

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally, amewataka mashabiki wa klabu hiyo kuwa wavumilivu katika kipindi ambacho timu hiyo inapitia wakati mgumu.


Ahmed Ally ameyasema hayo kupitia mtandao wa Instagram ambapo ameeleza kuwa "Dhahabu hupitishwa kwenye moto mkali ili ipate thamani na iwe bora, licha ya kuwa huteseka inapopita kwenye moto huo lakini mwishoe hubaki safi, bora na thamani yake huongezeka maradufu".


"Wana Simba tuvumilie kupita kwenye moto huu mkali ili tuwe bora na hadhi yetu irejee, najua maumivu ni makubwa kwa kuwa moto mkali lakini hatuna budi kuvumilia kwani ndio njia pekee ya kurudi kwenye thamani yetu" Ameeleza Ahmed

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad