Taarifa Mpya Kutoka TMA, Hali Mbaya ya Hewa Kwa Siku Tano...




Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetoa taarifa ya matarajio ya hali mbaya ya hewa kwa siku tano kuanzia saa 9:30 mchana wa leo Jumanne Aprili 16, 2024.
TMA imetoa tahadhari ya upepo mkali unaozidi kilomita 40 kwa saa na mawimbi makubwa yanayozidi mita mbili, kwa baadhi ya maeneo ya ukanda wa pwani ya Bahari ya
Hindi.
Maeneo hayo ni ya mikoa ya Dar es Salaam, Tanga, Pwani (ikijumuisha visiwa vya Mafia), Lindi na Mtwara pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad