Kocha Mgunda Atunisha Misuli SIMBA, Adai Mechi na Azam ni Fainali Kwao

 

Kocha Mgunda Atunisha Misuli SIMBA, Adai Mechi na Azam ni Fainali Kwao

kaimu Kocha Mkuu wa Klabu ya Simba, Juma Mgunda amesema kuwa anaamini ataisaidia timu hiyo kurejea katika makali yake ambayo imeyapoteza kwa siku za hivi karibuni baada ya kutetereka na kutopata matokeo chanya.

Mgunda ambaye amechukua mikoba ya Benchikha amesema hayo leo wakati akizungumza kwenye mkutano na wanahabari kuelekea mchezo wa kesho dhidi ya Azam Fc.

“Tunakutana na Azam FC, mchezo utakuwa mgumu sana na tunaweza kusema ni fainali kwa sababu ndio unaotoa taswira ya kushika nafasi ya pili kwa sababu tunahitaji kumaliza kwenye nafasi hiyo.

“Si rahisi, lakini naamini nitaisaidia Simba SC irudi kwenye ushindani, nina imani wachezaji watairudisha timu sehemu nzuri. Vijana waliopo wote wamepevuka na wanaelewa namna ya kufanya ili kuiweka timu katika ushindani, hivyo cha muhimu ni kuwajenga kisaikolojia na kuwarudisha kwenye morali na kila kitu kitakuwa sawa,” amesema Mgunda.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad